Psalms 53

Uovu Wa Wanadamu

(Zaburi 14)

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi.

1 aMpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa,
hakuna hata mmoja atendaye mema.

2 bMungu anawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.
3 cKila mmoja amegeukia mbali,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!

4 dJe, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwiti Mungu?
5 eHapo waliingiwa na hofu kuu,
ambapo hapakuwa cha kutetemesha.
Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia;
uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.

6Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni!
Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
Copyright information for SwhNEN